Tanzania itakuwa mwenyeji wa maadhimisho ya 6 ya wiki ya Maji Barani Afrika na Mkutano wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Nchi za Afrika yatakayofanyika Julai,2016 Jijini Dar es salaam.
Mkutano huo utahusisha washiriki zaidi ya 1000 kutoka mataifa 54 kutoka Bara la Afrika na wengine kutoka nje ya Afrika.
Kauli mbiu ya kongomanao hilo ni “ Kufikia lengo la maendeleo Endelevu Juu ya usalama wa Maji na usafi wa mazingira” – Matemu.