Kumekuwa na matukio mbalimbali ya utekaji nyara matukio hayo yamekuwa yakitishia usalama wa raia katika maeneo mbalimbali.

Mara nyingi watekwaji wamekuwa ni watu maarufu, wanasiasa, watoto, wasanii na wanawake na wamekuwa wakitekwa mara kwa mara kwa sababu ya pesa, kisasi,  fidia au imani za kishirikiana zinazohusiana na ukatwaji wa viungo vya binadamu na hili hutokea haswa kwa watoto na wanawake.

Na watekwaji wanaweza kurudishwa wakiwa wazima au maiti inategemea na matakwa ya watekaji hao.

Hivi karibuni nchini Tanzania kumekuwa na matukio ya utekaji yaliyotikisa nchi kisiasa, kiuchumi na kijamii hali iliyopelekea hofu kubwa kutanda miongoni mwa raia.

Tazama hapa matukio makubwa yautekaji yaliyotikisa dunia.

FC Barcelona wahimizwa kupambana bila Lionel Messi
Sijawahi kuomba kujiunga CCM, Polepole ni muongo- Komu