Meya wa Jiji la Dar es salaam, Isaya Mwita ametolea ufafanuzi taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kukamatwa kwa gari lake katika ofisi za chama cha mapinduzi wilaya ya Kinondoni.

Amesema kuwa maeneo kama hayo huwa yanalaza magari hivyo hapakuwa na nia yeyote ya kufanya uhalifu katika ofisi hizo.

Ameyasema hayo hii leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa hizo, ambapo amesema kuwa yeye ni mstaarabu wala hawezi kufanya chochote kibaya.

“Niwaondoe wasiwasi kuhusu dereva wangu, hakuwa na nia yeyote ya kufanya uhalifu, dereva wangu ni mtumishi wa umma na pale wanalaza magari ya binafsi na ya umma, hivyo pale aliona kuwa ni sehemu salama ndio maana akapaki pale,”amesema Mwita.

Aidha, ameongeza kuwa yeye hana nia mbaya na mgombea wa ubunge wa chama cha mapinduzi CCM, Maulid Mtulia kwani yeye kazi yake ni kuleta maendeleo ya jiji la Dar es salaam.

Magazeti ya Tanzania leo Januari 30, 2018
Rais Magufuli akutana na Dkt. Slaa Ikulu, wateta