Msanii wa muziki wa Taarabu nchini Canada kutoka Tanzania, Omary Niyonzima (Papa Fololo) ameitangaza kazi yake mpya inayokwenda kwa jina Msaliti. Omary  ni Mtanzania kutoka katika familia ya mzee Ally huko Uvinza, Kigoma ambaye aliimbia Band mbali mbali za muziki Tanzania kama TOT na nyingine, hivi sasa anaishi nchini Canada akifanya muziki wa asili ya Tanzania (muziki wa pwani). Bofya hapa kuitazama video ya wimbo wake mpya
Kama ilikupita hii video: Omary Mtanzania anayeimba Taarabu Canada, asimulia muziki huo unavyokubalika Canada