Rais Yoweri Museveni amemulikwa na vyombo vya habari nchini humo baada ya kumpandisha vyeo jeshini mwanae siku chache baada ya kuapishwa kuongoza kwa awamu ya tano.

Kwa mujinu wa Daily Monitor ya Uganda, Muhoozi Kaneirugaba mwenye umri wa miaka 42, alipandishwa kuwa Meja Jenerari. Pia, alipewa nafasi ya kuwa Kamanda wa Kikosi Maalum cha kumlinda Rais Museveni.

Kijana huyo wa Museveni alipandishwa vyeo pamoja na maafisa wengine wanne wa Jeshi la Uganda.

Museveni ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 71 aliapishwa hivi karibuni baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu uliopita, hivyo kuongezewa na wananchi kipindi alichokaa madarakani kufikia miaka 35.

 

Maduka, Magari yanayowakataa wana CCM yafungiwa, Maalim Seif Asema neno
Marekani wafanikiwa kupandikiza Uume unaofanya kazi