Serikali imekabidhi kiasi cha shilingi mil. 60 kwa Familia ya msanii maarufu nchini marehemu mzee Majuto ‘King Majuto’ kiasi ambacho alikuwa ameingia mikataba ya matangazo na makampuni mbalimbali.

Akikabidhi hundi hiyo, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wasanii wananufaika na sanaa zao.

”Lengo letu kubwa ni kuweza kuhakikisha wasanii wetu wananufaika na kazi zao, wanapata haki zao kama tulivyoweza kulisimamia suala hili la marehemu Mzee Majuto pamoja na Marehemu Kanumba,” amesema Dkt. Mwakyembe

 

Suarez awachana wachezaji wa Barcelona, Ronaldo de Lima naye asiliba kuhusu Messi
Serikali yakataza askari kutesa watuhumiwa