Serikali imesema  matumizi ya Teknolojia  ya Habari ya Mawasiliano (TEHAMA) hususani kompyuta yanazidi kukua  kwa kasi kubwa  duniani na hapa nchini, aidha shughuli nyingi za uendeshaji  wa ofisi  za Serikali na  na sekta binafsi, kama vile kuchapisha taarifa  mbalimbali za  mawasiliano ya kuhifadhi nyaraka zinafanywa na TEHAMA.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa udhibiti  wa huduma  za serikali mtandao, Michael Moshiro alipokuwa akiongea na waandishi wa habari mapema hii leo, amesema kuwa, pamoja na Serikali kubwa ambayo Serikali imeipata  katika matumizi ya TEHAMA kwa kipndi kirefu, bado kulikuwa na changamoto ambazo zilikwamisha malengo yaliyokusudiwa kwa haraka.

Aidha, Moshiro amezitaja changamoto hizo ni pamoja na utengezaji au ununuzi wa mifumo ya TEHAMA isiyozingatia mahitaji ya taasisi na serikali kwa ujumla, mifumo isiyoweza kubadilisha taarifa,uwepo wa urudufu wa mifumo na taarifa  zinazohifadhiwa na mifumo mbalimbali na rasilimali  za TEHAMA yasiyoshirikishi.

Hata hivyo amesema changamoto hizo zilipelekea serikali kutengeneza miongozo na viwango dhabiti   itakayowezesha  serikali kukabiliana nazo,na kuongeza kuwa  serikali ina lengo la kusaidia matumizi ya TEHAMA kwa usahihi

Video: Kampuni ya DataVision International kuongeza ufanisi katika sekta za kifedha
Video: Nchi iko hatarini kuwa jangwa - Makamba