Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wananchi kulipa kodi kwa muda ili iweze kufikia malengo iliyojiwekea katika kufikia maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Huduma na elimu kwa Mlipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa wananchi hawana budi kulipa kodi kwa muda.

“Niwakumbushe wananchi, wafanyabiashara kutoa risiti pindi wanapouza bidhaa kwani ni kitu cha msingi sana, hata wananchi nao wakumbuke kudai risiti kwakua ni haki yao,”amesema Kayombo

Video: Magufuli 'awakaanga' mawaziri wake wawili, Mvua yazua kizaazaa Dar
Magazeti ya Tanzania leo Januari 9, 2018