Vifaa vya kupigia kura vimewasili katika ya kaunti ya Kakamega nchini Kenya kwa maandalizi ya uchaguzi wa ugavana utakaofanyika Agosti 29, 2020.

Kwa mujibu wa  Msimamizi wa Urejeshaji wa IEBC Joseph Ayata vifaa vyote vitakuwa katika maeneo ya bunge ifikapo Jumapili alasiri katika matayarisho ya zoezi hilo ambalo litawawezesha wapiga kura kuamua mrithi wa Gavana Wycliffe Oparanya.

Takribani wapiga kura 844,709 mjini Kakamega watachagua nani kati ya Cleophas Malala wa ANC, Fernandez Baraza wa ODM, Cyrus Jirongo wa UDP na Samuel Omukoko wa chama cha MDP atakuwa Gavana katika mji huo.

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) pia itasimamia uchaguzi wa ugavana katika Kaunti ya Mombasa, uchaguzi wa Wabunge katika Majimbo ya Kitui Vijijini, Kacheliba, Pokot Kusini na Rongai.

Uchaguzi wa Wadi za Wabunge wa Kaunti pia utafanyika Kwa Njenga na Nyaki Magharibi.

Posho za wabunge zafyekwa
Bilionea mpya wa madini ya Tanzanite