Vigogo watano wa Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi (WETCU), wamehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka minne kila mmoja, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili likiwemo la kukisababishia chama hicho hasara ya zaidi sh. milioni 109.

Vigogo hao ambao walitiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Tabora, mbele ya Hakimu Mkazi, Tengwa Chiganga na kupewa adhabu hiyo, watatumikia kifungo cha miaka miwili gerezani kutokana na adhabu za kifungo.

Waliotiwa hatiani na kupewa adhabu hiyo ni  pamoja na aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mkandala Mkandala, Kaimu Meneja Mkuu, John Kusanja, Mhasibu mkuu, Prosper Mbacho, Francis Mpeta na  Makamu Mwenyekiti, Msafiri Ngassa ambao walipelekwa katika gereza la Uyui kuanza kutumikia adhabu ya kifungo.

Aidha, mahakama hiyo iliwaachia huru washitakiwa wawili katika kesi hiyo, Hamza Kapela na mfanyabiashara, Faraz Abbas ama Faraz Yaseen Abbasi, kutokana na upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Hata hivyo, washitakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashitaka manne ambayo ni kula njama ya kutenda kosa, kughushi, matumizi mabaya ya madaraka kwa kununua gari aina ya Toyota Land Cruiser V8 bila kupata kibali kutoka kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini na kukisababishia chama hicho hasara ya sh. 109,010,000 kutokana na kununua gari  hilo.

Uganda kununua boti za wagonjwa wa ajali za majini
Mtolea aanza kuuvizia ubunge, asema hana ugomvi na wabunge wa upinzani