Baadhi ya Wanawake nchini Morocco, wameandamana nje ya Bunge katika mji mkuu Rabat, wakitaka kuhalalishwa kwa suala la utoaji wa mimba wakitaka suala la kuwa na mtoto, liwe ni hiari.

Maandamano hayo ya Siku ya Kimataifa ya Utoaji Mimba kwa Usalama yalikuja wiki kadhaa baada ya msichana kijana, Meriem, kufariki katika kijiji kimoja katikati mwa nchi kufuatia kusitishwa kwa siri.

Uavyaji mimba ni kinyume cha sheria nchini Morocco, na unaadhibiwa kwa hadi miaka mitano jela, isipokuwa katika hali ambapo afya ya mwanamke iko hatarini.

Baadhi ya Wanawake walioandamana nchini Morocco kudai uhalali wa kutoa mimba. Picha na usatoday.

Huku wanaharakati hao, wakimheshimu kijana huyo kwa mabango yanayosema ‘Sote ni Meriem’, waliwataka wabunge kufanya uamuzi wa kuahirisha mimba kuwa chaguo la kisheria kwa wanawake.

Mwanaharakati, Sarah Benmoussa amesema, ‘Kuna wengi wanaokufa kila mwezi, kila mwaka kwa sababu hiyo, kwa sababu ya utoaji mimba kwa siri, na hawasikilizwi, hata kufikiriwa hawaheshimiwa, kama leo tunamheshimu Meriem na wale waliokufa kama yeye.”

Naye mwanafunzi wa uandishi wa Habari, Mis Khaoula (23), amesema, wanajaribu pia kuweka mazingira dhabiti na yenye afya kwa wanawake wengine wote ambao wanaweza kujikuta katika hali hiyo hiyo, wakiwa na ujauzito usiohitajika huku akidai kila binadamu anapaswa kuwa na uwezo wa kudhibiti mwili wake.

GGM yajitosa udhamini maonesho Teknolojia ya Madini
TEHAMA yaipaisha Tanzania uchumi kidijitali