Baraza Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi (CUF) Linalomuunga Mkono Prof. Ibrahim Lipumba limewavua uanachama Wabunge 8 wa Viti Maalum na Madiwani 2 wa chama hicho kwa kosa la kukisaliti chama.

Wabunge hao 10 na madiwani wawili wa CUF, wanaomuunga mkono, Katibu Mkuu, Seif Shariff Hamad jana waliiitwa kwa ajili ya mahojiano katika Ofisi za Chama cha Wananchi (CUF) lakini walikaidi wito huo wa kutokuonekana katika ofisi hizo.

Aidha, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi (CUF) limewavua uanachama wabunge wanane wa chama hicho kwa madai ya utovu wa nidhamu, yakiwemo kukisaliti chama hicho.

Mwenyekiti wa CUF, anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amesema, baraza pia limewavua uanachama madiwani wawili wa viti maalumu mkoani Dar es Salaam, kwa makosa kama hayo.

JPM: Nitachomoa mwingine mwenye akili kutoka upinzani
Lissu arudishwa rumande, tarehe ya hatma ya dhamana yake yatajwa