Mkutano Mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliokuwa ufanyike mwezi Disemba mwaka jana sasa utafanyika wikiendi hii Jumamosi na Jumapili tar 12-13 March 2016 jijini Tanga.

Ajenda za mkutano huu ni kwa mujibu wa katiba ya TFF. Mkutano mkuu utahitimishwa kwa uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha kukuza na kuendeleza vipaji vya uchezaji mpira, kituo kitakachojengwa jijini Tanga.

Mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa hoteli ya Regal Naivera.

Mohamed Mkopi Ni Bora Kuliko Wengine Kwa Mwezi February
597 Waliotimuliwa Kazi NIDA ‘wawaka’, waingia barabarani kudai milioni 900