Daraja la Wami, zimetokea ajali mbili za tofauti kwa kufuatana mara baada ya malori hayo kufeli breki na kusababisha vifo ambapo Lori la kwanza limesababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi wawili, huku lori la pili likiwa limesababisha vifo vya watu wawili mama pamoja na mtoto mdogo.

Katika ajali ya Lori la kwanza lililokuwa linatokea Dar es salaam kuelekea Arusha limepoteza mtu mmoja ambae alikuwa dereva aliyeshindikana kuokolewa kufuatia kwamba alikuwa amefunga mkanda wa gari hivyo amezama katika mto wami wenye kina kirefu pamoja na lori hilo.

Ajali hizo zimetokea June 5, 2020, ambapo wakati watu wakiwa wamejaa kushuhudia ajali hiyo ya lori, ghafla lori lingine pia likafeli breki na kusababisha vifo vya watu wawili ambao ni mama na mtoto waliokuwa kwenye eneo la tukio wakishangaa ajali ya kwanza ya lori.

Lakini pia Lori hilo limezoa magari zaidi ya saba ambayo yote yameharibiwa vibaya.

Aidha, jeshi la Uokaaji kwa kushirikiana na timu ya Askari polisi Wilayani bado wapo kwenye jitihada za kuhakiksha wanaokoa mwili wa dereva uliozama pamoja na lori mtoni.

Man Utd na Real Madrid zagongana kwa Lautaro Martinez
Magufuli atuma shukurani kwa viongozi wadini kwa kupambana na Corona