Watanzania watashuhudia moja kwa moja michuano ya kombe ya Afrika (AFCON) 2017 kupitia king’amuzi cha DSTV kwenye kifurushi cha bei nafuu cha Bomba

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Multichoice Tanzania, Salum Salum amethibitisha kuwa king’amuzi cha DSTV kitaonesha michuano hiyo mubashara kupitia channel yake ya Supersport4 (DSTV 204) ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kuiona michuano.

Salum amesema hayo katika tukio la kumkabidhi bendera ya Taifa mwanamuziki wa kizazi kipya, Nasibu Abdul (Diamond Patnumz) aliyepata mwaliko wa kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano ya AFCON 2017, nchini Gabon.

Video: Mjema agawa vyandarua Ilala, asisitiza wananchi wazingatie matumizi yake
Video: Maneno ya Diamond kuhusu kutumbuiza AFCON 2017 Gabon