Waziri wa ujenzi uchukuzi na mwasiliano profesa Makame Mbarawa Leo amezindua safari za train ya kutoka Dar es salaam  kwenda Pugu ilikukabiriana na tatizo la usafiri jijini.
Akizungumza katika  uzinduzi huo Mbarawa amesema  kuwa train hiyo itakuwa na uwezo wa kubeba
nakusafrisha abiria  1500 kwa awamu moja,na itakuwa na safari 3 kwa siku, na kuongeza kuwa train hiyo itakuwa inasafirisha watu 9000 kwa siku.
Aidha aliongeza kuwa serikali inafanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuanzisha usafiri wa boat kutoka posta hadi kijichi kwa ajili ya wakazi wa maeneo hayo.
Hatahivyo amewataka wananchi wote waliojenga maeneo ya hifadhi ya reli  kunodoka mara moja kabla hawajachukuliwa hatua za kisheria na kuwataka pia wafanyakazi wote  wanaofanya kazi kwa mazoea kuacha tabia hiyo  kwa kuwa serikali ya awamu ya tano haita mvumilia mfanyakazi mzembe.