Hakuna binadamu aliyewahi kufanikiwa kwa kuogopa kusemwa, kuchekwa, kupuuzwa,
Ila wapo waliofanikiwa kwa kuvumilia maneno, dharau, na kejeli
ukihitaji kufikia malengo yako usimwangalie mtu mwangalie Mungu na weka mkazo katika malengo yako.
Ijapokuwa wapo watu wenye imani juu nyota nzuri na nyota mbaya ndio chanzo cha mafanikio, la hasha juhudi na jitihada zako katika kazi ndio msingi mkubwa wa mafanikio, kwani mafanikio yako hayaletwi na mtu mwingine bali na wewe mwenyewe.