Wizara ya Fedha na Mipango imeliomba Bunge kuidhinisha Shilingi 15.94 trilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha bungeni bajeti ya wizara hiyo makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Amesema, kiwango hicho cha fedha Shilingi 15.38 trilioni, ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Shilingi 564.22 bilioni ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Makamu wa Rais aahidi huduma bora za Afya kwa Wananchi
Ange Postecoglou: Heshima ya Spurs inarudi