Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa Miguu Wilaya ya Mjini Hassan Haji “Chura” amesikitishwa kwa kutojumuishwa hata mjumbe mmoja kutoka chama chao kuwemo kwenye kamati inayosimamia kombe la Mapinduzi ambapo chama chao ndio waanzilishi wa Kombe hilo.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa Mwenyekiti huyo kwa kusema kuwa wao ndio walioanzisha kombe hilo lakini wamesahauliwa sasa.

“Nasikitika sana kuona katika wajumbe wote wa kamati ya kombe la Mapinduzi hata mjumbe mmoja kwetu hajatoka wakati sisi ndo waasisi wa kombe hili!”.

Aidha mwenyekiti huyo alizidi kufafanua juu ya kutoshirikishwa.

“ Ligi zipo nyingi lakini mbona watu wanakuwa vinganganizi kwenye kombe la Mapinduzi!, basi waiboreshe ligi kuu!, kwanini huko hawajenda?, kwasababu kombe la Mapinduzi ni biashara na linawanufaisha watu wengi”.Alisema Hassan.

Huu utakuwa ni mwaka wa tano kwa kombe hilo tangu liondoshwe ZFA Wilaya ya Mjini na kupelekwa Wizarani ambapo ZFA Wilaya ya Mjini walilianzisha mwaka 2007.

Ame Msimu: Mafunzo Bingwa Kombe La Mapinduzi
Sir Alex Ferguson Kurejea Man Utd