Maisha ya mapenzi ya kweli ni yale yaliyo na furaha pande zote mbili na kwamba kila mmoja anaridhika na mwenzi wake kwa hali na mali.

Mapenzi kama yanavyosemwa na watu ni sanaa kama sanaa zingine zilivyo. Kama ni mchezo, basi una sheria zake. Leo nakuonyesha mbinu ambazo ukizingatia ndoa yako haitokuwa na matatani.

Ni maoni tofauti tofauti kutoka kwa wadau pamoja na wazoefu wa masuala haya ya mahusiano.

Upendo
Kila mwanaume anataka kujisikia anapendwa. Anataka kuona kuwa mwenza wake anampenda kiuhalisia na anamjali wakati wowote.

Heshima
Hata pale anapokuwa hayupo, anataka mwenzake wake awe nyuma yake, kumuongelea na kumheshimu.

Kukubalika
Kila mwanaume anataka kujisikia mwenza wake anamkubali na kumthamini kwa mambo mbalimbali kama vile penzi lake, muda, jitihada, anavyojituma na kila anachokifanya kwa mwenza wake.

black-couples

Yeye ni bora zaidi
Anataka mwenza wake kujisikia kuwa yeye ni bora zaidi. Kila mwanaume anataka ajisikie kuwa yeye ni mwanaume bora zaidi kuliko wote aliowahi kuwa nao, na wengine wanataka kujisikia kuwa ni mwanaume pekee ambaye umewahi kuwa naye hata kama anajua si kweli.

Uaminifu
Mwanaume anahitaji mwenza wake awe mwaminifu. Uaminifu husaidia kujenga mapenzi zaidi, kila kitu kwa mwanaume na kadiri mwenzake anavyokuwa mwaminifu, ndivyo hawezi kuwa na wivu kwani anakuwa ameshajiaminisha.

Ukweli
Kila mwanaume anahitaji kujua kuwa anaweza kumwamini mwenza wake na kwamba naye anamwamini, ukiwa mkweli ni rahisi mume kukujengea imani, kuwa mkweli kwa kila jambo.

Aenda Jela kwa Kudanganya Kwenye Mtihani India, Sheria hii Ianze Tanzania?
Mbeya City Waachana Na Haningtony Kalyesubula