Kampuni ya Reli ya Tanzania (TRL) imefanya mabadiliko ya ratiba ya Treni ya Abiria kuelekea katika mikoa ya Kigoma na Mwanza kuanzia tarehe 02/8/2016 Treni itaanza kuondoka saa tisa mchana badala ya saa 11 jioni muda wa sasa.
Hayo yametangazwa na Meneja Uhusiano wa TRL Midladjy Maez wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake leo Jijini Dar es Salaam.
Maez amesema kuwa mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa treni ya pili ya huduma za Jiji kutoka kituo Kikuu cha Reli cha Dar es Salaam kwenda Pugu ambayo itaanza kutoa huduma mapema siku ya Jumatatu ya tarehe 01/08/2016.
Aidha aliongeza kuwa mabadiliko hayo yanahusu treni za abiria za huduma za kawaida zinazoondoka siku za Jumanne na Ijumaa na kuwa kwa upande wa huduma za treni ya Deluxe zitaendelea na muda wake wa kawaida.

Uongozi wa TRL umeamua kufanya mabadiliko hayo kwa sababu za kiusalama zaidi kwani mabadiliko haya yataepusha muingiliano usiokuwa wa lazima  na unaoweza kupelekea ajali na kuongeza kuwa kwa safari za kutoka Kigoma na Mwanza muda ni uleule. Alisema Maez.

Hata hivyo Meneja Uhusiano  aliongeza kuwa huduma za treni ya Jiji kwenda Pugu itakuwa na vituo 10 ambavyo ni pamoja na Pugu Stesheni, Gongo la Mboto,FFU Mombasa, Banana, (njia panda kwenda Stesheni), na karakata.
Vingine ni pamoja na Vingunguti Mbuzi,SS Bhakressa, Kamata na Kituo Kikuu cha reli Dar es Salaam.
Huduma hiyo itakuwa na awamu mbili asubuhi na Alasiri ambapo treni ya kwanza itaondoka kituo cha Pugu saa 12 asubuhi na kuwasili kituo cha Dar es Salaam sa 12:55 asubuhi na kufanya safari tatu zitakazomalizika saa 05:15 asubuhi. Jioni kutakuwa na safari tatu ambapo treni itaondoka kituo cha Dar es Salaam saa 09:55 alasiri kwenda Pugu na kuwasili saa 10:50 jioni na safari ya mwisho kutoka Pugu kuja Kituo Kikuu cha Dar es Salaam saa 03:20 usiku

Uchaguzi Wa Viongozi Wa Soka Bagamoyo Wapigwa Stop
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI