Bradley Barcola alifunga bao zuri sana katika mechi ya tatu ya mechi ya Ligue 1 dhidi ya Lille, akipokea pasi kutoka kwa Marco Asensio, na kufikisha mabao manne katika mechi tatu. Nyota huyo ameendelea kuwa na  kiwango kizuri tangu alipojiunga PSG . Staili yake ya kiuchezaji akitokea winga wa kulia na winga wa kushoto na mshambuliaji wa kati amekuwa bora kiuchezaji kitu  ambacho kinawafanya mashabiki wa Paris kuweka matumaini makubwa kwake.

Barcola ametimiza miaka 22 na amekwishacheza michezo 29 akiwa na uzi wa PSG akifunga mabao 8. Kuondoka Kylian Mbappe kunamfanya nyota huyu ajihakikishie nafasi ya kwanza kwenye kikosi cha PSG na kocha Luis Enrique ameonekana kuvutiwa na kijana huyo anayechipukia. Wadau wengi wanaamini nyota huyo ni mrithi sahihi wa Mbappe na kama atapata wasaa zaidi wa kucheza basi atakuwa mchezaji tegemeo kwa siku za mbeleni.

Bradley Barcola ni nani?

Bradley Laurent Barcola (aliyezaliwa 2 Septemba 2002) ni mchezaji wa soka wa Ufaransa ambaye anacheza kama mshambuliaji au winga wa klabu ya Ligue 1 ya Paris Saint-Germain na timu ya taifa ya Ufaransa.

Baada ya kuingia katika akademi ya Lyon, Barcola alianza kazi yake ya kitaaluma na klabu yake ya utotoni, ambapo angecheza misimu miwili, ambayo mwishowe aliingia kwenye kikosi kilichoanza, akiiongoza klabu hiyo katika kutoa pasi za mabao. Uwezo mzuri aliouonyesha ulipelekea uhamisho wa euro milioni 45 kwenda Paris Saint-Germain mnamo Julai 2023.

Barcola ilichezea Ufaransa soka la kimataifa la vijana chini ya umri wa miaka 21 na viwango vya Olimpiki. Alicheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa mnamo Juni 2024, na alikuwa mmoja wa wachezaji wa kikosi cha Ufaransa kwa UEFA Euro 2024.

Guardiola afunguka hatma ya Foden timu ya taifa
Ukame wasitisha mauzo ya Nafaka nje