Mchezaji wa klabu ya Simba Jean Ahoua amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji Bora wa mwezi Agosti baada ya kuisaidia Simba kushinda mechi zake mbili za ligi kuu ya NBC.

Ahoua amehusika katika magoli manne Kati ya 7 yaliyofungwa na Simba kwenye mechi hizo akitoa pasi tatu zilizozaa  mabao na bao moja alilofunga.

Kocha Fadlu ameibuka mshindi wa kocha Bora wa mwezi akiisaidia Simba kushinda mechi mbili na kufunga mabao 7 huku timu yake ikiwa haijaruhusu bao lolote

Hii hapa barua kutoka Bodi ya ligi

Wazazi hakuna akili za kurithi - DAS Nguya
Singida BS watolea ufafanuzi ishu ya Chasambi