Na Humphrey Edward.

Ni nani alikuwa Mtu wa kwanza kuitawala Amerika? Maana hadi miaka michache iliyopita, iliaminika kwamba utamaduni wa kwanza wa Marekani ulikuwa ni ule wa Clovis, wa mababu wa Wenyeji wa Amerika Kaskazini.

Zaidi ya hayo, pia ilifikiriwa kwamba wanadamu walifika katika bara hilo miaka 14,000 iliyopita, kwa hiyo, katika “ujenzi” huu wa historia, ustaarabu wa kwanza ungekuwa wa Amerika Kaskazini, wakati Waaztec, Maya na Incas wangekuja baadaye sana.

Ugunduzi wa hivi majuzi, pamoja na uchanganuzi wa DNA, umeangazia jinsi akiolojia ilivyokuwa na makosa, ikiarifu kwamba ustaarabu wa kwanza wa Amerika walikuwa watu wa Amerika ya Kati na Kusini, angalau miaka 15,000 – 20,000 ikiwa ni mapema kuliko ilivyoaminika hapo awali.

Na watu hawa walikuja kwa usafiri wa Baharini (ndiyo, ni sahihi, “walikuja kwa Bahari”), kutoka Siberia na Sundaland (bara ambalo lilitoweka, hadithi ambayo inafanana na ile ya Indonesia ya sasa na visiwa vya jirani).

Hivi karibuni mwaka 2020, Watafiti wengine walichapisha matokeo ya ugunduzi wa mabaki ya binadamu katika pango la Chiquihuite, huko Mexico, lakini uchimbaji huo ulianza mwaka2012 na ule wa kina zaidi ulifanywa mnamo mwaka 2016 na 2017.

Habari hiyo, ilichapishwa katika jarida la Nature na kilichopatikana kwenye pango kilibadilisha kabisa maoni ya wanaakiolojia ambapo utafiti huo uliowasilishwa na Mwanaakiolojia katika Chuo Kikuu cha Autonomous cha Zacatecas Nchini Mexico, Prof. Ciprian Ardelean na wenzake, ukisema watu waliishi katikati mwa Mexico angalau miaka 26,500 iliyopita.

Profesa huyo alisema, “inachukua karne nyingi, au milenia, ili watu wavuke Beringia na kufika katikati ya Mexico.” Baadaye, anaongeza hivi: “Inachukua miaka mingi ya kuwapo hapo awali ili kuwafikisha huko iwe walikuja kwa bahari au nchi kavu.” Hii ina maana kwamba huenda wanadamu walikuwa Amerika ya Kati muda mrefu kabla ya miaka 30,000 iliyopita.

Lakini si hayo tu, kwani Kituo kingine cha utafiti kimegundua kwamba wakazi asilia wa Amerika ya Kati na Kusini hawana babu mmoja, bali wana wawili. Hao kiuhalisia wanatambuliwa kama wana watu mama na idadi ya watu Y na ambao ni wenyeji wa asili wa Sundaland kutoka zamani za mbali, huku pia wakiwa na “watu wa baba”, ambao ni Inupat, wanaotoka Siberia.

Ugunduzi huu kimsingi hubadilisha imani zote za kiakiolojia kuhusu siku za nyuma za Amerika. Na hapa ndipo linapokuja swali kuwa nani aliyekuwa mmiliki wa magofu ya kale zaidi yaliyopatikana katika nchi hizo wakati huo? Ni ustaarabu gani wa zamani uliweza kuunda geopolymers juu ya Andes?

Nani aliunda michoro kubwa ya Nazca na juu ya yote kwa madhumuni gani? Na zaidi ya yote ikiwa miaka 30,000 iliyopita watu waliweza kusafiri kutoka Australia hadi Amerika ya Kati, ni nini kiliwazuia kutoka Amerika ya Kati hadi Misri, kama ushahidi mbalimbali unavyoonekana sasa? Nafuatilia nitarudi kwa andiko jingine.

Dkt. Biteko: Tanzania ni familia, itajengwa na Watu wote
Mramba awakaribisha Waingereza uwekezaji Nishati jadidifu