Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesisitiza umuhimu wa elimu ya amali kama njia ya kukuza ujuzi wa kiutendaji katika sekta mbalimbali kama vile ufundi, kilimo, uvuvi, muziki na michezo.
Aidha, ametoa wito kwa wazazi na wawekezaji kuunga mkono elimu hiyo kwa kuwa ni suluhisho muhimu kwa changamoto ya ukosefu wa ajira na inahitajika kwa ufanisi wa sekta ya uwekezaji.
Prof. Mkenda ameyasema hayo , katika Mkutano wa Umoja wa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Ameeleza kuwa shule za amali zitakazokuwa na rasilimali na vitendea kazi vya kutosha zitapata kibali cha kufundisha na kutoa mafunzo ya vitendo.
Pia, amesisitiza kuwa elimu ya amali inapaswa kuimarishwa ili kukabiliana na upungufu wa wafanyakazi wenye ujuzi katika sekta mbalimbali za uchumi.
“Wazazi kumsihofie kupeleka watoto wenu katika shule za amali, elimu hii ni fursa muhimu ya kuwajengea watoto maisha bora na mustakabali mzuri wa ajira,”amesema.

BRELA yafuta usajili wa Makampuni 11 Nchini
Hali ya Papa Francis yazidi kuimarika - Vatican