Chama cha ACT Wazalendo kimeitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kufafanua tukio la kuzuiliwa kwa Viongozi lililotokea nchini Angola na msimamo wa Serikali juu ya suala hilo.
Tamko hilo limekuja baada ya viongozi wa vyama mbalimbali kuzuiliwa kuingia jijini Luanda kwa ajili ya kushiriki mkutano kuhusu masuala ya demokrasia akiwemo kiongozi wa chama hicho, Dorothy Semu.
Wengine waliozuiliwa ni pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Othman Masoud.