Chuo cha Ufundi Stadi (VETA), Songea imedhamiria kuibua vipaji na kuwafundisha misingi ya maisha Watoto, kupitia programu ya kona ya watoto.
Hayo yamebainishwa na Mwalimu kutoa VETA Songea, Faulata Mutalemwa katika maonesho ya 49 ya Kimataifa yaBiashara a yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba Temeke Jijini Dar es salaam.
Amesema kupitia kona hiyo, watoto watajifunza vitu mbalimbali ikiwemo stadi za mikono mbalimbali na kuondoka nazo ikiwemo
ushonaji, urembo na ufundi wa umeme.
“Mtoto anaweza kujifunza vitu mbalimbali vya namna ya kuchana nywele, kutunza ngozi yake, namna ya kushona nguo zake pamoja na kudhiifadhi,” alisema Mutalemwa.