Muigizaji na Mtangazaji maarufu wa Ukraine Pasha Lee, 33 aliyekua akiigiza sauti katika michezo ya Maigizo ameuwawa katika vita inayoendelea kati ya Urusi na Ukraine kwa siku ya 13 sasa.

Siku tano zilizopita kwa mujibu wa jarida la habari la Daily Mail, Pasha aliweka picha katika mtandao wake akiwa amevalia mavazi ya Kijeshi na kuandika ‘Tuungane Pamoja’.

Picha yake ya Mwishoni kwa siku mbili zilizopita aliyokuwa amehusishwa na Irpen iliandikwa ‘kwa masaa 48 yaliyoisha tunapata wasaa wa kuouga picha na kuonesha tulivyopigwa mabomu na bado tunatabasamu na ni kwa sababu tutashinda’