Klabu ya YoungA fricans italazimika kumkosa kiungo wake, Salum Aboubakar ‘Sure Boy’ kutokana na kadi aliyoipata katika mchezo dhidi ya Geita Gold FC, Jumapili (Machi 06) kwenye Uwanja waCCM Kirumba Jijini Mwanza.

Kadi hiyo inamfanya kiungo Salum Abubakar ‘SURE BOY’ akose mchezo unaofuata wa Ligi Kuu dhidi ya KMC FC ambao utapigwa March 16 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam.

Sure Boy amefikisha kadi tatu za Njano ambapo alipata katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar na Biashara United na Geita Gold FC.

Kiungo Khalid Aucho anatarajiwa kurejea kikosini katika mchezo dhidi ya KMC FC baada ya afya yake kuimarika kama ilivyo kwa Saido Ntibazonkiza, Djuma Shabani na Chico Ushindi.

Sure Boy anatarajia kurejea kikosini kuwakabili waajiri wake wa zamani Azam FC katika Mchezo utakaopigwa Azam Complex, April 06.

Ngariba Simanjiro wajisalimisha, wakabidhi visu vya kukeketea
?rane: Hakuna asiyependa kufanya kazi Simba SC