Baada ya kuzindua matoleo mapya ya simu za Samsung S23 (Galaxy S23 Ultra | S23 Plus na S23). @Samsungtanzania imeendelea kusogeza experience premium ya simu hizi kwa kupitia wahamisashaji kama @IdrisSultan, @FahadFuad na @IreneKiwia ili kuelezea wateja mapya ya simu hizi zenye teknolojia ya hali ya juu.

Simu hizi zina uwezo wa kupiga picha zenye quality kupitia kamera zake zenye hadi mega pixel 200. Pia picha zinaweza kuvutwa kwa ukaribu hata ikiwa mita mbali kutoka kwa kamera hii. Vile vile Kamera ina uwezo wa kutoa picha na video ang’avu nyakati za usiku.

Idris, Fahad na Irene kwa pamoja wamezungumzia ubora wa simu hizi za Samsung Galaxy S23 Series kwa kuonesha ubora na wa muonekano ya simu zenyewe zinazopatikana katika rangi 4 tofauti, Galaxy S23 inakuja na S-Pen inayoweza kurahisisha matumizi ya kuchkua taarifa, uwezo wa kucheza game na marafiki pamoja na uwezo wa kamera kupiga picha nyakati za usiku.

Fahad pia amevutiwa kufanya kazi na Samsung hasa kwa mazingatio ya utengenezwaji wa Simu hizi za Samsung Galaxy S23 series, unaojali utunzwaji wa mazingira ili kuyahifadhi. Hii ni kuanzia malighafi zinavyopatikana, uzalishwaji, usambazaji pamoja uwezo wa kuchakata upya ni moja ya mazingation ya Samsung katika kutengeneza simu hizi.

CPB yanunua Mazao ya Bilioni 9.6, yazalisha tani 1000
Kocha Pluijm anaitaka Young Africans Nusu Fainali