Mabingwa wa Soka nchini Ufaransa Paris Saint-Germain wamemsajili beki Lucas Hernandez kutoka FC Bayern Munich kwa mkataba wa miaka mitano, mabingwa hao wa Ligue 1 wametangaza.

Ada ya uhamisho haijaweka wazi, lakini vyombo vya habari vya Ufaransa viliripoti kuwa PSG walikuwa wameilipa Bayern ada ya euro milioni 40 pamoja na nyongeza kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27.

“Nimefurahi sana! Nimekuwa nikisubiri kujiunga na PSG kwa muda mrefu na hatimaye imetokea. Ni siku maalum sana kwangu na nina furaha sana kuwa hapa,” alisema Hernandez katika taarifa yake.

Atletico Madrid, klabu ya utotoni ya Hernandez, pia itapokea gawio la ada kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Hispania.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alicheza mechi 107 kwa mabingwa hao wa Ujerumani tangu kuwasili kwake mwaka 2019, lakini alicheza mechi saba pekee za ligi msimu uliopita baada ya kupata jeraha la mguu kwenye Kombe la Dunia ambalo lilimfanya kuwa nje kwa muda uliosalia wa msimu.

Hernandez, mchezaji mpya wa tano kusajiliwa PSG, anaungana na viungo Manuel Ugarte na Lee Kang-in, beki wa kati Milan Skriniar na fowadi Marco Asensio.

Klabu hiyo pia ilimtimua kocha Christophe Galtier na nafasi yake kuchukuliwa na kocha wa zamani wa Barcelona na Hispania, Luis Enrique.

Wengine watatu kutambulishwa Simba SC
Haya hapa malengo ya Singida Fountain Gate