Kiungo kutoka nchini England James Maddison amesema angependa Harry Kane abaki Tottenham Hotspur lakini amesisitiza kuwa uvumi unaoendelea kuhusu Mshambuliaji huyo haujawasumbua wachezaji wenzake wapya.

Maddison alikua mmoja wa wachezaji wa kwanza kusajiliwa chini ya kocha mpya, Ange Postecoglou pale Spurs ilipokamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 40 kutoka Leicester mwezi uliopita.

Majuma matano yamepita na bado mustakabali wa Kane haujajulilkana, huku Mabingwa wa Ujerumani FC Bayern Munich wakiwa na nia ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa England na wanatarajiwa kuwasilisha ombi jipya kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30.

Mwenyekiti wa Spurs, Daniel Levy aliripotiwa kukutana na naofisa wa bva hivi majuzi ya mjini London Jumatatu na klabu hiyo katika bara la Asia-Pacific ilitokea huku kukiwa na mazunngumzo mara kwa mara kuhusu mustakabali wa Kane, na mwandishi wa habari wa Bild alithibitisha jezi ya Bayern na Kane yenye namba 9 ngongoni kwa Postecoglou wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Lakini Maddison, akizungumza kwenye hafla ya kuanza msimu alisema: “Haijakuwa kikwazo, Harry ni mtaalamu wa hali ya juu.

“Sitaelezea kwa undani kwa sababu sijui chochote na tuwe na heshima kuhusu hali ya Harry.

“Kila mtu anajua Harry Kane ni mtu wa namna gani, yeye ni mtaalamu wa hali ya juu, wakati wowote anapoingia kwenye mazoezi hutoa asilimia ya nguvu zake.

“Ningependa Harry Kane abaki. Yeye ndiye namba tisa bora zaidi duniani kwa maoni yangu, lakini itakuwaje akiondoka?

Goncalo Ramos kumbadili Mbappe PSG
Al Ahli kumsajili Franck Kessie