Kocha Mkuu wa Singida Fountain Gate, Hans Van Pluijm amesema ameridhishwa na kiwango cha wachezaji wake na sasa wapo tayari kuikabili Simba SC kwenye mchezo wao wa Ngao ya Jamii utakaofanyika Alhamis (Agosti 10) kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga.

Pluijm amesema kiwango walichokionyesha wachezaji wake kwenye mchezo wao kimataifa wa kirafiki dhidi ya AS Vita uliochezwa Jumatano(Agosti 02) kimemfurahisha na kumemuaminisha kuwa sasa wapo tayari kwa ligi kuu na michezo yote iliyopo mbele yao.

Kocha huyo kutoka Uholanzi amesema wachezaji wake walicheza mechi hiyo kwa bidii na kujituma, hivyo ana uhakika kama wataendelea kucheza hivyo kwenye mechi zinazofuata hana shaka na ushindi kwani anaviamini viwango vya wachezaji wake.

Al Ahli kumsajili Franck Kessie
Minziro matarajio kibao Ligi Kuu 2023/24