Mahakama ya uchaguzi wa Rais nchini Nigeria, imetupilia mbali hoja za wapinzani kupinga ushindi wa Rais Bola Tinubu katika uchaguzi mkuu uliofanyika Februari 2023 kufuatia Atiku Abubakar wa People’s Democratic Party na Peter Obi wa Labour Party, walioshika nafasi ya pili na ya tatu mtawalia, walikuwa wameiomba mahakama kufuta uchaguzi huo, kwa madai ya kuwepo kasoro wakati wa uchaguzi.

Majaji wa mahakama hiyo ya watu watano, wakipokezana kusoma hukumu kwa zaidi ya saa 11, walikataa maombi ya kibinafsi ya Atiku na Obi, ambapo Jaji Haruna Tsammani alisema ombi la Obi halikuwa na maana na halikuwa na ushahidi wowote wa kuaminika wa kutosha kuunga mkono madai ya ukiukwaji wa sheria.

Tsammani alisema madai ya Atiku ya ulaghai wa kura yalikuwa ya na mapungufu na akapuuza hoja yake kwamba Tinubu hakuwa na sifa za kuwania urais, ambapo Obi na Atiku, ambao hawakuwa mahakamani, hawakuweza kupatikana mara moja ili kutoa maoni yao. Chama cha Labour cha Obi katika taarifa kilikataa uamuzi huo na kusema kitatangaza hatua zake zinazofuata baada ya mkutano na mawakili.

Katika taarifa kutoka India ambako anajiandaa kushiriki katika mkutano wa G20, Tinubu alikaribisha uamuzi wa mahakama hiyo na kuwataka wapinzani wake na wafuasi wao kuunga mkono serikali yake na hata hivyo, uchaguzi huo uliibua dalili ndogo ya kuibuka kwa upinzani maarufu, na Tinubu amekubaliwa na jumuiya ya kimataifa kama kiongozi halali wa Nigeria.

Hata hivyo, Atiku na Obi wanaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Juu ya nchi hiyo kutupilia mbali uamuzi wa mahakama hiyo. Rufaa yoyote lazima ikamilishwe ndani ya siku 60 tangu tarehe ya hukumu ya mahakama na hakuna pingamizi la kisheria katika matokeo ya uchaguzi wa rais ambalo limewahi kufanikiwa nchini Nigeria.

TAMISEMI yatakiwa kukamilisha maboma Sekta ya Afya
Mbappe aacha njozi nzito Real Madrid