Licha ya kuwahi kucheza na Power Dynamos ya Zambia na kupata matokeo mazuri, lakini Kocha mkuu wa Simba, Roberto Oliviera ‘Robertinho’ anaendelea kuwafatilia kwa umakini wapinzani wao hao.

Simba SC inaendelea na maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Power Dynamos, utakaopigwa Jumamosi (Septemba 16), katika uwanja wa Levy Mwanawasa, Zambia.

Kocha Robertinho amesema kuwa amewapa wachezaji wake kutoka Zambia mbinu za kuwa wanaijua vizuri timu hiyo na wanachopaswa kufanya kuelekea katika mchezo huo.

Amesema wamefanikiwa kucheza na timu hiyo kwa kushinda anaimani katika mechi ijayo watakuja kivingine na kuwatumia wachezaji hao kutoa siri za Power Dynarmos.

“Haitakuwa mechi rahisi, kama tuliwafunga katika tamasha letu haitaleta maana kuwa watakuwa wepesi, ninaimani watakuja tofauti na vile walivyocheza awali kwa sababu haya mashindano.

“Binafsi presha kwa sababu tunao wachezaji wengi ambao wanawajua wapinzani wetu ambao tumecheza nao kabla ya msimu kuanza, lakini tunaamini watakuwa wamebadilika hivyo hawa ambao tupo nao naamini watatusaida,” amesema Robertinho.

Habibu Kondo: Tutachukuwa alama tatu Dodoma
Serikali kushirikisha Mashirika ya Kimataifa Sekta ya Nishati