Shirikisho la Soka Barani Afrika ‘CAF’ limepanga Makundi ya Kombe la Shirikisho Barani humo msimu huu 2023/24, huku mchaka mchaka kwa timu shiriki katika hatua hiyo ukitarajiwa kuanza Novemba 26.

CAF imepanga makundi hayo mjini Johannesburg-Afrika Kusini leo Ijumaa (Oktoba 06), chini na Mkuu wa Idara ya Mashindano ya Shirikisho hilo, Khalid Nassar.

Bingwa wa michauno hiyo msimu wa 2022/23 USMA Algers kutoka Algeria amepangwa Kundi A sambamba na Future (Misri), Super Sports United (Afrika Kusini) na Al Hilal (Libya).

Kundi B: Zamalek SC (Misri), Sagrada Esperança (Angola), Académie SOAR (Guinea) na Abu Salim (Libya).

Kundi C: Rivers United (Nigeria), Club Africain (Tunisia), Dreams FC (Ghana) na Académica do Lobito (Angola).

Kundi D: RS Berkane (Morocco), Diables Noirs (Congo Brazzaville), Stade Malien (Mali) na Sekhukhune United (Afrika Kusini).

Arafat Haji: Tumepoteza Mechi sio Ubingwa
Wakuu wa Mikoa watii agizo la Prof. Ndalichako