Al-Ittihad wametangaza kumsajili Danilo Pereira kutoka Paris Saint-Germain.Kiungo huyo ambaye mara nyingi alikuwa akitumika kama beki wa kati wa PSG, amehamia Saudi Pro League kwa mkataba unaodaiwa kuwa na thamani ya Euro milioni 5.

Pereira alicheza mechi 157 kwa mabingwa hao wa Ufaransa katika mashindano yote kwa miaka minne, akishinda mataji matatu ya Ligue 1, Coupe de France mara mbili, na Trophee des Champions mara tatu.Hata hivyo, hakupendelewa, kwa kuwa hajashiriki katika kikosi chochote cha Luis Enrique katika mechi yoyote hadi sasa kwamsimu huu.Pereira alikuwa na vizuizi vingi (25) kati ya wachezaji wa PSG kwenye ligi msimu uliopita, na alimaliza pasi nyingi zaidi (2084), huku akishinda mipira mara 128, akiwa namba nne kwa wachezaji bora wa timu ya PSG.

Al-Ittihad pia wamethibitisha kuwasili kwa Steven Bergwijn kutoka Ajax kwa dau la €25m. Winga huyo, ambaye alijiunga na Ajax Julai 2022, alicheza mechi 80, akifunga mabao 31 na kusajili mabao 41.

 

TAMWA ZNZ yataka adhabu kali kwa wanaodhalilisha Watoto
Kane ataweza kuvunja rekodi za Lewandowski?