Afarah Suleiman, Babati – Manyara.

Chama cha Mapinduzi – CCM, Mkoa wa Manyara kimewataka Wananchi kujitokeza kujiandikisha katika taftari la makazi linalotarajiwa kuanza kesho Oktoba 11 – 20, 2024.

Wito huo Umetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Manyara, Peter Toima wakati akizungumzia zoezi hilo katika mkutano wake na Waandishi wa Habari mjini Babati.

Amesema, kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la makazi kutawasaidia Wananchi kupiga kura na kuwachagua Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa katika Uchaguzi huo unaotarajia kufanyika Novemba 27, 2024.

Hata hivyo, Toima ametoa wito kwa wasomi wenye sifa za kiuongozi kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali kupitia chama hicho katika mchakato wa ndani wa chama kuanzia Okotba 20 – 24, 2024.

Kibaha: Shule ya Uongozi, Chuo Renmin kubadilishana wataalamu
Makala: Pogba anapouchekea Ubaya Ubwela