Chama cha ACT – Wazalendo kimetoa tamko la kulaani tamko la Serikali kupitia Waziri wa Habari, Utamadauni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kuwa TBC haitarusha Live mkutano wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tamko hilo la ACT -Wazalendo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Samson Mwigamba limekiita kitendo hicho kuwa cha aibu na kinacholenga kuminya demokrasia nchini.

Hili ndilo tamko la ACT- Wazalendo:

JANA limetokea tukio la aibu katika nchi yetu pale serikali ilipofanya jaribio la hatari la kuzuia wananchi kuona na kusikia kinachoendelea bungeni.

Kitendo cha serikali ya CCM kuzuia kuonyeshwa moja kwa moja vipindi vya bunge katika televisheni ya taifa ni cha kijima na sisi chama cha ACT-Wazalendo tunakilaani kwa nguvu zetu zote.

Tunakitafsiri kitendo hiki cha serikali kama mwendelezo wa hatua na juhudi za Rais Magufuli za kuminya demokrasia na kusimika utawala wa kiimla.

Tunawasihi wananchi kusimama imara na kuzipinga jitihada zozote ovu za kuminya demokrasia nchini.

Tunawapongeza wabunge wazalendo wa upinzani kwa kusimama pamoja na kupinga nia ovu ya serikali ya kuua demokrasia katika nchi yetu.

Tunawatia shime wabunge wote wazalendo kuendelea kupigania maslahi mapana ya taifa letu.

ACT-Wazalendo! Taifa kwanza leo na kesho!

Imetolewa na;

Samson Mwigamba,

KATIBU MKUU.

Bweni la Shule ya Sekondari ya Lowassa yateketea kwa moto
Rais Magufuli amteua naibu Gavana wa benki kuu