Trent Alexander-Arnold amekiri kuwa hajui nafasi yake bora ya kucheza baada ya kutumia muda katika safu ya kiungo msimu huu 2023/24.

Kiungo huyo wa kati katika siku zake za akademi, alifanywa kuwa beki wa kulia na Liverpool, lakini maswali juu ya uwezo wake wa ulinzi yamewafanya Kocha wa Wekundu hao, Jurgen Klopp na wa kikosi cha England, Gareth Southgate, kumtumia mbele zaidi katika safu ya kiungo.

Baada ya kuanza kuelekea mwisho wa msimu uliopita kama mbinu ya kurekebisha kiwango cha klabu, Alexander-Arnold amecheza kama kiungo.

Wote Klopp na Southgate watalazimika kuamua ni wapi mustakabali wa muda mrefu wa Alexander-Arnold upo na mchezaji mwenyewe amekiri kuwa hajui anapaswa kucheza wapi.

“Watu wanaona uwezekano wa mimi kuwa na ufanisi zaidi katikati ya uwanja,” alisema.

“Hiyo labda ni njia ya kwenda mbele. Lakini nani anajua? Si uamuzi wangu. Ninaweza kuchezeshwa tu katika nafasi niliyoambiwa.

Akitafakari juu ya uhamisho wake wa awali chini ya Klopp msimu uliopita, Alexander-Arnold aliongeza: “Wakati kocha alinionesha jukumu lililopinduliwa, niliona kama fursa ya kuonesha ninaweza kucheza katikati ya uwanja.

Unaweza kupata mchezo mmoja, haifanyi kazi ukiwa umetoka kucheza maisha yako yote katika nafasi ya beki wa kulia.”

Puuzeni, hakuna kiwanda cha kutengeneza Mayai - Serikali
Umati wa Rais Samia tishio kwa upinzani 2025