Timu ya Mafunzo ya mpira wa Wavu yapania kuchukuwa ubingwa wa Mapinduzi yatakayoanza tarehe 6/1/2016 katika uwanja wa Mafunzo Mjini Unguja.

Kauli hiyo ameitoa kocha wao Mkuu ambae ni Ame Msimu alipozungumza nasi leo hii asubuhi baada ya kumaliza mazoezi.

“ Maandalizi mazuri na vijana wanapokea vizuri mazoezi na ndio maana naamini ntachukua Ubingwa wa Mapinduzi kama nilivyochukuwa ubingwa wa ligi kuu”. Alisema Ame.

Mapinduzi Zanzibar huwa yanaenda sambamba na michezo mbali mbali kila ifikapo mwezi Januari ambapo vyama vya michezo tofauti huandaa mashindano yao kwa mchezo husika kwa kwenda sambamba na kuazimisha sherehe hizo.

Ndege yaahirisha safari Kwa Kumuogopa Panya
ZFA Wilaya Ya Mjini Walia Na Kombe La Mapinduzi