Rais Samia Suluhu Hassan leo Machi 4, 2022 amekutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe.

Rais Samia Suluhu akizungumza na Mwenyekiti wa CHADEMA

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kurugwnzi ya mawasiliano Ikulu leo, Rais Samia amesisitiza kuwa kuna umuhimu wa kushirikiana ili kuijenga Tanzania kwa kuaminiana na kuheshimiana kwa misingi ya haki.

Aidha, taarifa imesema kuwa Freeman Mbowe amemshukuru Rais Samia kwa kuonesha kujali huku akikubali kuwa msingi mkubwa wa kujenga taila la Tanzania ni kusimama katika haki.

Vile vile, amesema wamekubaliana kufanya siasa za kistaarabu na kiungwana na kuwa yuko tayari kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo ili nao pia waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Rais Samia aeleza walichozungumza na Mbowe Ikulu
Ajiua kwa kukimbia tuhuma za mauaji