Vurugu na sintofahamu imeibuka muda mfupi uliopita katika mkutano wa Bunge uliokuwa unaendelea mjini Dodoma.

Taarifa kutoka kwa waandishi wa habari waliokuwa ndani ya Bunge hilo zimeeleza kuwa polisi walilazimika kuingia ndani kuwatoa nje wabunge wa upinzani kufuatia maigizo ya mwenyekiti wa kikao hicho, Andrew Chenge, baada ya kukaudi amri ya kutoka nje.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa awali, wabunge wa upinzani walipinga kuendelea kwa mjadala wa Bunge wakitaka kauli ya Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na michezo, Nape Nnauye kuhusu TBC kutorusha ‘Live’ matangazo ya Bunge ijadiliwe kwanza.

Mwenyekiti wa Bunge alieleza kuwa huo haukuwa muda wa mjadala huo na kutaka Bunge liendelee na ratiba yake.

Hata hivyo, wabunge wanne pekee wa Upinzani ndio waliokuwa wametakiwa kutoka nje ya Bunge, lakini wabunge wote wa Ukawa waliwatetea na kuanza kuimba nyimbo mbalimbali. Hivyo, Mwenyekiti aliamuru wote watoke nje ili wabunge wengine waendelee kujadili hotuba ya Rais.

Mwandishi wa East Africa Radio aliyekuwa ndani ya Bunge alieleza kuwa Mwenyekiti wa Bunge aliondoka kwenye kiti chake wakati vurugu hizo zikiendelea na waandishi wa habari waliagizwa kutoka nje.

 

Serikali Yatoa Agizo La Mashirikisho Ya Michezo
Simba Waanika Wazi Msimamo Wao Kuhusu Ratiba Ya VPL