Nchi ya Burkina Faso imeanza maombolezo ya siku 3 ya kitaifa, baada ya kuuawa kwa watu 38 katika shambulio la kushtukiza lililotekelezwa na Wanajihadi wa Kiislamu Kaskazini mwa nchi hiyo.

Rais wa nchi hiyo, Roch Marc Christian Kabore amesema kilichotokea ni pigo kwa Taifa na kuwataka wananchi kuungana kuhakikisha wanayashinda makundi ya kijihadi.

Waziri wa Ulinzi wa Burkina Faso Moumina Cherif Sy anasema idadi ya waliouliwa kutokana na shambuliao la kigaidi karibu na mgodi wa dhahabu imefikia 38 na wengine 63 wamejeruhiwa.

Waziri Sy aliyetembelea eneo shambulio lilitokea katika jimbo la mashariki ya mji mkuu wa Wagadougou anasema maafisa wa uokozi wangali wanawatafuta wachimba migodi wengine ambao bado hawajulikani walipo.

Kampuni ya Canada ya Semafo inayosimamia kazi za mgodi huo imeeleza Ijumaa kwamba mabasi yake matano yaliyo kuwa yanawasafirisha wafanyakazi kuelekea kazini yalishambuliwa na wanamgambo wasiojulikana wa makundi ya wafuasi wa itikadi kali za Kiislamu yanayoendesha shughuli zake kaskazini na mashariki ya Burkina Faso.

Taifa hilo la Afrika Magharibi linalofahamika kwa utulivu wake limekuwa likipambana na mashambulizi ya kigaidi yaliyowasababisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao tangu mwanzoni mwa mwaka huu kulingana na mashirika ya kimataifa ya huduma za dharura.

Undani kisa cha Bibi aliyehukumiwa kunyongwa hadi kufa
Pompeo aadhimisha miaka 30 kuangushwa ukuta wa Berlin kwa lawama