Chama Cha Sanaa Mbeya – CHASAMBE, wameiomba Serikali na Jamii kuwatambua na kuwapa fursa mbalimbali Ikiwemo Kushiriki katika matamasha yanayohamasisha Maendeleo.

Akizungumza kwa niaba ya Wasanii wa Mbeya Mwenyekiti wa CHASAMBE, Farida Ngoyi amesema jamii na Serikali isiwape Wasanii wanaotoka Nje ya Mbeya kipaumbele  hasa kwenye Matamasha makubwa kwani kitendo hicho ni  kudhoofisha Sanaa ya Mbeya.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Beno Malisa amewaondoa hofu na kuwahakikishia Serikali  Itawaunga mkono na kwa katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane, yatakayofanyika Mbeya itawapa nafasi ya Kusherehesha na kuonesha vipaji vyao.

Aidha, amewataka kuongeza ubunifu huku akisema, “Sanaa ni nyenzo  kubwa inayotumika  katika Kuelimisha, Kufundisha na Kuonya hivyo basi itumieni  kukemea  vitendo vya mmomonyoko wa maadili na Ukatili wa Kijinsia.”

Malisa ameongeza kuwa, “Bila kusahau kutumia Sanaa  kuyasema makubwa yaliyofanywa na Serikali  ya awamu ya sita  kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mh Rais  Dkt Samia Suluhu Hassan.”

Chasambe Ni chama Chenye wanachama hai  616  chama hiko kina jumping Wasanii wa sanaa zote Wanaopatikana Jijini  Mbeya.

Uwekezaji, ulinzi wazikutanisha Tanzania, India
Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Julai 10, 2023