Christian Pulisic anaonekana kuwa na mwanzo mzuri zaidi kwenye Ligi Kuu Italia, Serie A, baada ya kufunga bao la pili kwenye mchezo wa pili mfululizo.

Baada ya kuifungia AC Milan bao la kwanza wikendi iliyopita, Pulisic pia alifunga katika mechi yake ya kwanza Uwanja wa San Siro na kuwafanya Rossoneri kuibuka na ushindi wa mabao 41 dhidi ya Torino juzi Jumamosi (Agosti 26).

Olivier Giroud alifunga Penati mbili na kufikisha mabao matatu katika mechi mbili za kwanza, huku Theo Hernández pia akifunga bao.

“Mechi bora, kazi ya kila wiki ilitufanya tuwe sawa,” alisema Pulisic akiiambia DAZN.

“Timu imefanya mchezo kuwa mzuri na uimarishaji wa hali ya juu umefika. Kundi zuri linaundwa kwa mtazamo, upatikanaji.”

Pulisic alihusishwa na mchezaji mwenzake wa zamani Giroud kufunga bao katika mechi yake ya kwanza huko Bologna na wakati huu alikuwa Ruben Loftus-Cheek aliyesaidia kutengeneza bao la kwanza dakika ya 33.

Pulisic alianza harakati hiyo katika eneo la kiungo kwa kumtengenezea mpira Loftus-Cheek.

Giroud hakuweza kuingia kwenye mkwaju, lakini ilimnjia Pulisic, ambaye alikimbia na kufunga bao la kwanza.

Pulisic na Loftus-Cheek walijiunga kutoka Chelsea mwezi uliopita.

Perr Schuurs alisawazishia Torino dakika tatu tu baadaye, lakini Giroud akarejesha bao kwa Milan kabla ya kipindi cha mapumziko kwa mkwaju wa penalti baada ya mlinzi wa Torino, Alessandro Buongiorno kucheza madhambi katika eneo la hatari.

Juanma Lillo ashusha Presha Man City
Walimu wathaminiwe: DC Hamid Seif