Klabu ya Schalke 04 ya nchini Ujerumani, imethibitisha kumsajili beki wa kulia kutoka nchini Hispania Jorge Andújar Moreno “Coke”, akitokea Sevilla CF.
Taarifa ya uthibitisho iliyotolewa na klabu ya Schalke, imeeleza kuwa, usajili wa beki huyo mwenye umri wa miaka 29, umewagharimu kiasi cha Euro milion 5.
.@SevillaFC_ENG right back #Coke passed a medical with #S04 on Sunday: https://t.co/pxpCUXVMWb pic.twitter.com/FARPyKBmV1
— FC Schalke 04 (@s04_en) July 31, 2016
Coke anaondoka nchini Hispania huku akikumbukwa alijiunga na Sevilla CF mwaka 2011 akitokea Rayo Vallecano, na alifanikiwa kuwa nahodha wa mabingwa hao wa Europa League mara tatu mfululizo.