Mashabiki wa klabu za Barcelona na Atletico Madrid wamelishutumu shirikisho la soka duniani FIFA, baada ya kutangaza orodha ya mwisho ya wachezaji watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa shirikisho hilo.

Luka Modric, Cristiano Ronaldo na Mohamed Salah wametajwa kuwania tuzo hiyo ya FIFA jana jumatatu, huku majina ya Lionel Messi na Antoine Griezmann yakiondolewa.

Mashabiki wa klabu hizo za Hispania wameonyesha hasira zao kupitia mitandao ya kijamii, ambapo wameeleza kuchukizwa na hatua hiyo kutokana na kuamini kuwa, wachezaji hao walipaswa kuwa miongoni mwa wanaostahili kuwania tuzo kwa mwaka huu 2018.

Mshabiki hao wameeleza kuwa, wachezaji hao wamekua katika kiwango cha hali ya juu msimu uliopita na wamezisaidia timu zao kufanya vyema katika ligi ya Hispania pamoja na michuano mingine, tofauti na Luka Modric, Cristiano Ronaldo na Mohamed Salah ambao watawania wapo kwenye orodha ya mwisho.

Mbali na orodha hiyo ya wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa FIFA kwa mwaka 2018, shirikisho hilo limetangaza orodha nyingine za watakaowania tuzo mbalimbali.

Tuzo Ya Kipa Bora

Thibaut Courtois (Real Madrid, Ubelgiji), Hugo Lloris (Tottenham Hotspur, Ufaransa) na Kasper Schmeichel (Leicester City, Denmark).

Tuzo Ya Kocha Bora Wa Kiume.

Zlatko Dalić (Croatia), Didier Deschamps (Ufaransa) na Zinedine Zidane (Real Madrid).

Mchezaji Bora Wa Kike.

Ada Hegerberg (Lyon, Norway), Dzsenifer Marozsán  (Lyon, Ujerumani) na Marta (United States Orlando Pride, Brazil).

Tuzo Ya Kocha Bora Wa Kike.

Reynald Pedros (Lyon), Asako Takakura (Japan)  na  Sarina Wiegman (Uholanzi).

Tuzo Ya Goli Bora.

Mchezaji Mchezo Mashindano Tarehe  
 Gareth Bale Real Madrid – Liverpool 2017–18 UEFA Champions League 26 May 2018
 Denis Cheryshev Russia – Croatia 2018 FIFA World Cup 7 July 2018
 Lazaros Christodoulopoulos AEK Athens – Olympiacos 2017–18 Superleague Greece 24 September 2017
 Giorgian De Arrascaeta Cruzeiro – América Mineiro 2018 Campeonato Mineiro 4 February 2018
 Riley McGree Newcastle Jets – Melbourne City 2017–18 A-League
 Lionel Messi Nigeria – Argentina 2018 FIFA World Cup 26 June 2018
 Benjamin Pavard France – Argentina 2018 FIFA World Cup 30 June 2018
 Ricardo Quaresma Iran – Portugal 2018 FIFA World Cup 25 June 2018
 Cristiano Ronaldo Juventus – Real Madrid 2017–18 UEFA Champions League 3 April 2018
 Mohamed Salah Liverpool – Everton 2017–18 Premier League 10 December 2017

Tuzo Ya Mashabiki Bora.

MAshabiki Mchezo Mashindano Tarehe
Sebastián Carrera Coquimbo Unido – Deportes Puerto Montt 2017 Primera B de Chile 22 October 2017
Mashabiki wa Japan na  Senegal 2018 FIFA World Cup June 2018
Mashabiki wa Peru 2018 FIFA World Cup June 2018

 

Hafla ya kutangaza washindi wa tuzo za FIFA kwa mwaka 2018 imepangwa kufanyika septemba 24 katika ukumbi wa Royal Festival jijini London, England.

Jean- Pierre Bemba akosa sifa za kugombea Urais Congo DRC
Video: DC Busega atangaza fursa 8 zakuchangamkia wilayani kwake