FC Barcelona imetangaza kupata faida kubwa ya jumla euro milioni 304 kwa msimu wa 2022/2023.

Mapato ya jumla ya uendeshaji yalikuwa euro bilioni 1.259, wakati gharama za uendeshaji zilikuwa euro bilioni 1.165.

Katika mitiririko ya kibiashara (euro milioni 350) na uuzaji (euro milioni 100), Barcelona ilifurahia rekodi za mapato.

Mikataba ya ufadhili pia iliwawezesha kupata euro milioni 200, iliyoboreshwa kwa kusajili washirika 20 wapya.

Kama ilivyothibitishwa hapo awali, klabu ilichangisha euro milioni 400 kwa kuuza asilimia 15 ya haki za sauti kwa matangazo ya La Liga.

Deni halisi limepungua tangu mwaka uliopita, sasa ni euro milioni 552 kutoka euro milioni 680.

Kushuka kwa deni la kumesababisha kushuka kwa deni la jumla la klabu hiyo.

Muhtasari kutoka katika klabu hiyo ulieleza: “Bodi imetathmini uwiano mzuri wa mwisho wa mwaka huu wa fedha, ambapo pia imeongeza hatua za kudhibiti na kupunguza matumizi ambayo yanatekelezwa tangu mwanzo wa mamlaka ya sasa mnamo mwaka 2021.”

Rais wa Barca, Joan Laporta hivi majuzi alidai ahueni ya kifedha ya klabu hiyo, ambayo imewakatisha tamaa katika misimu ya hivi karibuni, itamaliza mapema kuliko ilivyotarajiwa.

“Tunaboresha katika nyanja zote,” alisema.

“Sote tunadhani tuna kikosi kizuri sana mwaka huu, tunawapongeza wote wenye majukumu ya kimichezo, tumejitahidi sana kusajili wachezaji wote, tulioona watátufaa.

Uongozi Tabora Utd wamshangaa Asante Kwasi
Gamondi ashindilia msumari Ligi ya Mabingwa