Jarida la Forbes limetoa orodha ya waigizaji wa kike wenye kipato kikubwa zaidi duniani mwaka 2020.

Sofía Vergara aliyeshiriki kwenye tamthilia ya Modern Family ameshika nafasi ya kwanza kwenye orodha hiyo, lakini bingwa wa zamani Scarlett Johansson hajaingia orodha hiyo kwa sababu filamu yake Black Widow imeahirishwa kutolewa kutokana na janga la virusi vya Corona.

Waigazi wa kike walioingiza fedha nyingi zaidi kati ya Juni Mosi mwaka 2019 hadi Juni Mosi mwaka huu ni wafuatao:

  1. Sofía Vergara, dola za kimarekani milioni 43
  2. Angelina Jolie, dola za kimarekani milioni 35.3
  3. Gal Gadot, dola za kimarekani milioni 31.5
  4. Melissa McCarthy, dola za kimarekani milioni 25
  5. Meryl Streep, dola za kimarekani milioni 24.

Rage: Young Africans washtakiwe kisheria
FC Barcelona yapata hasara ya mabilioni